Chebukati: Mkurugenzi wa ICT, James Muhati atimuliwe
Published on: September 19, 2017 08:14 (EAT)
Uamuzi kamili wa mahakama ya upeo ukisubiriwa, mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Wafula Chebukati sasa anapendekeza kusimamishwa kazi kwa maafisa watatu wanaohusika na habari na teknolojia. Chebukati anasema kuwa uchunguzi wa ndani kwa ndani wa IEBC unaonyesha kuwa mkurugenzi wa habari na teknolojia James Muhati, mshirikishi Paul Mugo na Boniface Wamae walikiuka sheria katika utekelezaji wa majukumu yao na kusababisha makosa yaliochangia kubatilishwa kwa matokeo ya uchaguzi.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment