Jeshi lachukua mamlaka ya utawala jijini Harare
Published on: November 15, 2017 08:19 (EAT)
Hali si hali nchini Zimbabwe baada ya wanajeshi kuchukua hatamu za uongozi wa nchi hiyo siku moja tu baada ya mkuu wa wanajeshi kutangaza kuwa hawataruhusu viongozi waliopigania uongozi wa taifa hilo kunyanyaswa na maafisa wachache wa chama tawala cha ZANU-PF. Haya yanajiri siku chache baada ya makamu wa rais Emmerson Mnangagwa kufutwa kazi kwa madai ya kutaka kumwondoa mamlakani Rais Robert Mugabe.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment