Jubilee wakataa maafisa waliotajwa na Chebukati

Mirengo ya Jubilee na Nasa inazidi kuzozana kuhusu maandalizi ya uchaguzi mpya wa urais, kama ilivyoagizwa na mahakama ya juu nchini. Jubilee imepinga mabadiliko ya uongozi katika secretariat ya IEBC, na kudai Marjan Hussein aliyeteuliwa kuongoza shughuli za kinyang’anyiro kipya cha ikulu ni mshirika wa karibu wa Nasa. Kwa upande wake, Nasa inashinikiza kuondolewa kabisa kwa afisa mkuu mtendaji wa IEBC Ezra Chiloba na wakurugenzi sita wa IEBC, na pia kuhusishwa katika upekuzi wa mitambo ili kufanikisha uchaguzi huru na haki.

Tags:

Uhuru kenyatta IEBC raila odinga JUBILEE NASA Raphael Tuju Wafula Chebukati Ezra Chiloba

Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories