Jubilee wawinda kura Kitale, Kericho na Narok
Published on: July 29, 2017 08:29 (EAT)
Chama cha Jubilee kimetetea rekodi yake uongozini kwa muhula wa miaka minne, na kuwarai wakenya kuchagua kati ya maendeleo na porojo. Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto wamefanya msururu wa mikutano kaunti za Trans Nzoia, Narok na Kericho, huku wakiutaja muungano wa upinzani-Nasa kama kongamano la viongozi walio na kiu ya utawala lakini hawana dira ya maendeleo na utangamano wa kitaifa.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment