Korti yasitisha pendekezo la kupunguza mishahara ya wabunge
Published on: December 15, 2017 07:50 (EAT)
Mahakama kuu imesitisha kwa muda, utekelezaji wa utaratibu wa kupunguza mishahara na marupurupu ya wabunge ulioasisiwa na tume ya mishahara nchini (SRC). Jaji George Odunga alitoa agizo hilo baada ya tume ya huduma za bunge (PSC) kuwasilisha kesi, na kudai SRC iliwadhulumu wabunge na haikuzingatia gharama yao ya maisha ilipopiga wembe mishahara yao. Kando na kupokea mshahara wa takriban shilingi milioni moja kila mmoja, wabunge sasa wataweza kupokea marupurupu ya usafiri, magari na mikopo ya nyumba.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment