Maadhimisho ya wiki nzima ya walemavu yakamilika

Umati wa watu wakiwemo walemavu wa kusikia walikusanyika hii leo katika uwanja wa Railway Football Club hapa jijini Nairobi ili kuadhimisha siku ya walemavu wa kusikia ulimwenguni.
Leo ikiwa ni mwisho wa maadhimisho ya wiki moja kuhusu walemavu wa kusikia ulimwenguni, walikusanyika kufanya matembezi ya Amani kutoka jumba la KICC hadi uwanja wa Railway football club.
Kampeni hizi za watu walio na ulemavu wa kusikia unalenga kuhamasisha wananchi kuhusu umuhimu wa kujua lugha ya ishara na kuwatambua watu wanaoishi na ulemavu katika katiba ya taifa hili.

Tags:

walemavu sign language ulemavu

Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories