Mazungumzo ya kutatua mgomo wa madaktari yaongezewa muda
Published on: March 02, 2017 09:11 (EAT)
Viongozi wa kidini sasa ndio wanaoendesha mkutano wa kutafuta suluhu ya mgomo wa madaktari baada ya mahakama kuwaruhusu siku mbili walizoomba ili kukamilisha mazungumzo ambayo tayari walikuwa wameanzisha. Viongozi hao leo wamekutana na madaktari na kesho watafanya mkutano la tume ya kukadiria mishahara ya umma, tume ya wafanyikazi wa umma, chama cha madaktari na serikali ili kukamilisha mazungumzo hayo. Ripoti yao itawasilishwa mahakamani Jumanne.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment