Pembe za ndovu zenye thamani ya Ksh 2 M zanaswa Kwale
Audio By Vocalize
Maafisa wa polisi huko Kwale wamenasa kilo 41.9 za pembe ya ndovu zinazokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi milioni mbili.
OCPD wa Msambweni Josephat Chebusit, amesema kwamba pembe hizo zilipatikana nyumbani mwa mama mmoja katika eneo la Msambweni. Aidha imebainika kwamba pembe hizo zilikuwa zimekatwa katwa kwa vipande themanini na nane na kupakiwa kwenye magunia kadhaa. Uchunguzi wa kubaini waendeshaji wa biashara ya aina hiyo tayari umeanzishwa katika eneo hilo.

Join the Discussion
Share your perspective with the Citizen Digital community.
No comments yet
This discussion is waiting for your voice. Be the first to share your thoughts!