Rais aomba Wakenya waunge SRC mkono
Published on: July 11, 2017 08:55 (EAT)
Rais uhuru Kenyatta amesifia na kuunga mkono hatua ya tume ya kutathmini mishahara na marupurupu ya wafanyakazi wa umma nchini SRC ya kupunguza kiwango cha mishahara wanachopokea wafanyakazi wa umma. Kenyatta pia amewaomba Wakenya kwa jumla kuiunga mkono tume hiyo akieleza kwamba taifa litanufaika pakubwa kutokana na fedha za ziada zitakazopatikana ambazo pia amesema zitatumika pakubwa kuimarisha uchumi wa nchi.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment