Rais atoa wito wa amani nchini
.Je, tume ya uchaguzi nchini-IEBC iko tayari kusimamia uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti kwa njia huru na haki? Ndiyo kitendawili washikadau mbali mbali walikongamana kutegua leo, huku Rais Uhuru Kenyatta na mpinzani wake mkuu, kinara wa NASA Raila Odinga wakichukua misimamo tofauti. Ingawa kenyatta anaahidi kuheshimu uamuzi wa wakenya na kung’atuka iwapo atabwagwa kwenye mchuano ujao, anawataka wapinzani wake kuheshimu Uhuru wa IEBC, na kutoingilia majukumu yake. Lakini kwa upande wake, Odinga anasema IEBC ina njama fiche, huku akisisitiza zabuni ya uchapishaji wa karatasi za kupigia kura iliyopewa kampuni ya Al Ghurair ibatilishwe, na kutangazwa upya.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment