Serikali kununua vitabu vya kusoma mwakani
Published on: December 04, 2017 08:26 (EAT)
Wanafunzi wa kidato cha kwanza watapata vitabu sita vya masomo ya lazima (core subjects) kuanzia Januari mwaka ujao kutoka kwa wizara ya elimu. Waziri wa elimu Fred Matiang’i ametangaza mwamko huo mpya akisema shule hazitapokea tena pesa za kununua vitabu kwani kumekuwa na wizi na ufujaji wa hela za mpango huo. Waziri alisema hayo alipozindua shughuli ya kutoa nafasi za shule za upili kwa watahiniwa wa KCPE mwaka huu ambapo pia alitangaza mabadiliko kadhaa katika sekta ya elimu.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment