Uhuru amjibu Raila kuhusu madai ya wizi wa kura
Published on: July 28, 2017 08:30 (EAT)
Rais Uhuru Kenyatta amemsuta mgombea urais wa nasa Raila Odinga kwa kutupia tope jina la walinda usalama wa nchi na kudai kuwa watatumiwa katika njama ya wizi wa kura katika uchaguzi ujao. Rais amesema kuwa Odinga amewakosea heshima wanajeshi na maafisa wa polisi kwa matamshi kama hayo na kusema kuwa kila pingamizi wanalotoa wana Nasa linaashiria kuwa hawataki uchaguzi ufanyike tarehe nane mwezi ujao.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment