Wana-NASA wakaidi amri ya Matiang’i, wasema Ijumaa ni siku ya maandamano

Malumbano makali yananukia kesho kati ya waandamanani wa muungano wa upinzani –NASA – na maafisa wa polisi katika miji ya Nairobi, Mombasa na Kisumu baada ya viongozi wa muungano wa NASA kupuuzilia mbali maagizo ya kaimu waziri wa usalama Dkt Fred Matiang’i kutoa maandamana katikati ya miji hiyo. NASA wanasema kuwa maandamano yataendelea kama yalivyopangwa na kuwa Matiang’i hana mamlaka ya kuwanyima haki yao ya kuandamana. Hata hivyo viongozi wa Jubilee wamemuunga mkono Matiang’i na kusema kuwa wananchi, wafanyibiashara na mali yao wana haki ya kulindwa dhidi ya uharibifu wa waandamanaji.

Tags:

Fred Matiang'i NASA anti-IEBC protests

Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories