Waziri Amina ashindwa na waziri wa Chad
Published on: January 30, 2017 09:27 (EAT)
Kenya imepata pigo kubwa la kidiplomasia baada ya kukosa nafasi ya kuiongoza Kamisheni ya Umoja wa Afrika. Balozi Amina Mohammed ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya alikuwa miongoni mwa wagombea 5 wa nafasi hiyo yenye ushawishi mkubwa. Mousa Faki Mahamat amechaguliwa mwenyekiti mpya baada ya kujizolea kura 38 katika uchaguzi uliofanywa na mataifa ya Afrika huko Addis Ababa, Ethiopia.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment